OGAMBA AHIMIZA UTEKELEZAJI WA CBE
Waziri wa Elimu Julius Ogamba ametoa wito wa kuharakishwa kwa utekelezaji wa mfumo wa elimu unaozingatia ujuzi wa mwanafunzi, CBE.
Ogamba amesisitizaumuhimu wa mfumo huo katika kukuza ubunifu na kuwajengea wanafunzi ujuzi unaohitajika katika soko la ajira.
Wadau wa elimu pia wameitaka serikali kuunga mkono ubunifu na kuwekeza zaidi katika rasilimali na miundombinu ili kuhakikisha utekelezaji bora wa mfumo huo.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 




































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































