WAFANYAKAZI WATAKA “COTU’ MBADALA
Kundi la wafanyakazi nchini likiongozwa na aliyekuwa naibu rais Rigathi Gachagua, limependekeza kubuniwa kwa muungano mbadala wa vyama vya wafanyakazi kutoa ushindani kwa ule wa COTU, kwa misingi kwamba COTU imeshindwa kuwawakilisha wafanyakazi ipasavyo.
Miongoni mwa misingi ya kubuniwa kwa muungano huo ni madai kwamba katibu mkuu wa COTU Francis Atwoli, imeshirikiana na serikali ya Rais William Ruto licha ya serikali hiyo kuidhinisha kukatwa kwa makato wanayoyataja kuwa makubwa ya mishahara ya wafanyakazi.
Aidha, wamemtuhumu Atwoli kuwa mbinafasi.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 




































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































