MURUNGI AKOSOA BARAZA LA MAGAVANA

Naibu Spika wa Seneti na Seneta wa Meru, Kathuri Murungi, amelikosoa vikali Baraza la Magavana kwa kutishia kususia vikao vya Kamati ya Ukaguzi wa Hesabu za Umma, akiwataka waboreshe utendaji wao au waachie nyadhifa zao. Murungi amekanusha madai ya magavana kwamba wanatishwa au kunyanyaswa wanapofika mbele ya kamati za Seneti, akisisitiza kuwa ukaguzi wa matumizi […]

OBURU AONYA VIONGOZI WA ODM KUHUSU NIDHAMU

Kiongozi wa chama cha ODM, Oburu Oginga, amewakosoa vikali maafisa wakuu wa chama wanaodaiwa kukiuka maamuzi ya vyombo muhimu vya chama, akionya kuwa ukosefu wa nidhamu miongoni mwa uongozi unatishia mshikamano wa ODM. Akihutubia kikao cha Kamati Kuu ya Kitaifa (NEC) kilichofanyika Mombasa, Oburu amesema baadhi ya wanachama wa Kamati ya Utendaji na Kamati Kuu wamekuwa […]

SIFUNA AKOSA KIKAO CHA NEC YA ODM

Seneta wa Nairobi na Katibu Mkuu wa ODM, Edwin Sifuna, amekosa kuhudhuria kikao muhimu cha Kamati Kuu ya Kitaifa (NEC) kilichofanyika Mombasa hali inayochochea mjadala kuhusu mpasuko unaoendelea ndani ya chama hicho. Kikao hicho kilikuwa kimeitishwa na kiongozi ODM, Oburu Oginga, kujadili masuala ya uongozi wakati mazungumzo kuhusu uwezekano wa ushirikiano kati ya ODM na UDA […]

UNITED WAPATA ‘JERAHA’ LA KWANZA CHINI YA CARRICK

Bao la Benjamin Sesko katika dakika ya 96 liliihakiikisha Manchester United rekodi ya kutopoteza mechi chini ya kocha mshikilizi Michael Carrick, baada ya kulazimisha sare ya bao 1-1 ugenini dhidi ya West Ham United. Carrick alikuwa ameshinda mechi zote 4 tangu alipochukua hatamu Old Trafford, ila msururu wa ushindi mfululizo ulitiwa breki na nyundo la […]

LEOPARDS WATATOA TENA KUCHA, KOCHA AMBANI

Kocha mkuu wa AFC Leopards Fred Ambani ameelezea matumaini ya vijana wake kuonyesha kocha tena, baada ya kubanduliwa na timu ya BB Bread kwenye dimba la FKF Cup, akisema vijana wake wana uwezo wa kujikung’uta vumbi na kuangazia ubingwa wa KPL. Leopards wanajiandaa kwa mechi ya ligi ugenini dhidi ya Bandari FC katika uwanja wa […]

RISING STARLETS TANZANIA KWA MECHI YA KUFUZU WC

Kikosi cha timu ya taifa ya Kenya kwa wachezaji wasiozidi umri wa miaka 20 cha wanawake Rising Starlets, kinaendelea na mazoezi yake nchini Tanzania kujiandaa kwa mechi ya marudiano ya kufuzu dimba la kombe la dunia kwa wachezaji wa umri huo. Kwenye mechi ya mkondo wa kwanza Jumamosi iliyopita, vipusa hao wanaonolewa na Jackline Juma […]

6 WALIOKWAMA JENGONI OTC WAOKOLEWA

Wafanyakazi 6 waliokuwa wamekwama kwenye jengo lililoporomoka mapema leo wakati wa ujenzi kwenye barabara ya Kirinyaga katibu nae neo la OTC jijini Nairobi wameokolewa na vikosi vya uokoaji. Katika taarifa, shirika la Kenya Red Cross limesema vikosi vya uokoaji kutoka idara ya wazima moto ya kaunti ya Nairobi, Kituo cha kitaifa kuhusu operesheni za majanga, […]

UFADHILI FINYU KIZINGITI KWA SHA

Ukosefu wa ufadhili wa kutosha ni mojawapo ya vizingiti vikubwa vinavyozuia utekelezaji wa bima ya afya ya jamii SHA, bima iliyolenga kuleta suluhu kwa upatikanaji wa huduma za matibabu kwa wakenya. Kwenye ripoti yake, taasisi ya masuala ya uchumi nchini, IEA, imebainisha changamoto zinazozuia utekelezaji wa bima hiyo, ikisema licha ya mamilioni ya wakenya kusajiliwa, […]

VUTA NIKUVUTE KUVUTA NYUMA MAENDELEO

Huenda mvutano kati ya baraza la magavana na maseneta kuhusu madai ya ulaji rushwa yakaathiri utendakazi kwa wananchi mashinani, kamati ya seneti kuhusu uhasibu wa fedha za umma ikitishia kushinikiza seneti kusitisha mgao wa kaunti ambazo magavana wake watakosa kufika mbele ya kamati hiyo. Kamati hiyo inayoongozwa na seneta wa Homa Bay Moses Kajwang’, imepuzilia […]

MUDAVADI AKIRI WAKENYA WALILAGHAIWA URUSI

Serikali imekiri kuwa wakenya waliouawa kwenye vita kati ya Urusi na Ukraine walilagahiwa na mawakala waliowaahidi kazi nyingineza na wala si za kijeshi, ikisema inaelekea Urusi kubaini kinachoendelea. Akizungumza na shirika moja la habari la kimataifa, mkuu wa mawaziri Musalia Mudavadi, ambaye pia ni Waziri wa masuala ya kigeni, amesema ni wakenya 7 waliokwama katika […]