HAZINA YATAKA BUNGE KUFUNGUA FEDHA ZA UWEKEZAJI

Hazina ya Kitaifa imetetea hali ya uchumi wa Kenya na kutaka Bunge liende kwa kasi katika kuidhinisha vyombo muhimu vya kifedha vinavyokusudiwa kufungua fedha kuu za uwekezaji. Kupitia taarifa  kwenye mtandao X hapo jana, Hazina imesema viashiria vya hivi karibuni vya uchumi vinaonyesha utulivu unaokua, hata wakati ambao wabunge wanajadili mwelekeo wa kifedha wa nchi. Ni swala ambalo liliibuka wakati wa mkutano […]

PSG, REAL MADRID WASUBIRI DROO YA UEFA CL

Mabingwa watetezi wa dimba la klabu bingwa bara Ulaya PSG na miamba wa soka barani humo Real Madrid, ni miongoni mwa miamba wa soka duniani wanaosubiri kwa hamu kufahamu wapinzani wake katika mechi za mwondoano wa kutinga awamu ya timu 16 za mwisho za dimba hilo. Droo hiyo itaandaliwa hii leo, baada ya awamu ya […]

NAIBOIS KUANZA UTETEZI DHIDI LA L15 FC

Mabingwa watetezi wa taji la FKF Kenya Cup, Nairobi United, wataanza kampeni ya kutetea taji hilo dhidi ya L15 FC, inayoshiriki ligi la FKF kiwango cha kaunti ya Kilifi katika raundi ya timu 64 inayojumuisha timu kutoka ligii kuu hadi zile za mashinani. Naibois, jinsi wanavyofahamika, waliwabandua miamba wa soka nchini Gor Mahia kutwaa taji […]

SAWE KUTETEA UBINGWA WAKE LONDON

Bingwa mtetezi wa mbio za London Marathon Sabastian Sawe, ameratibiwa kutetea ubingwa wake katika mbio zitakazoandaliwa tarehe 26 Aprili, akiamini kuwa huenda akahitaji kuvunja rekodi aliyoandikisha ili atetee ubingwa wake kutokana na ushindani mkali. Mkenya huyo mwenye umri wa miaka 29, anatarajia ushindani kutoka kwa vigogo wenza akiwemo Jacob Kiplimo wa Uganda aliyemaliza wa pili […]

RUTO AWATAKA VIJANA KUKUMBATIA NYOTA

Rais William Ruto amewahimiza vijana kote nchini kukumbatia mipango ya ujasiriamali inayoendeshwa na serikali kama vile mradi wa NYOTA, kama njia mojawapo ya kuimarika kiuchumi. Akizungumza mjini Kisii wakati wa uzinduzi wa mradi huo kwa vijana kutoka kaunti ya Kisii, Migori na Nyamira , Rais Ruto amesema mradi huo ni sehemu ya ahadi zilizotolewa na […]

UCHUNGU WA SUKARI NCHINI

Imebainika kuwa serikali haijalipa deni la zaidi ya shilingi bilioni 10 kwa wafanyakazi wa viwanda vya sukari nchini, licha ya kutangaza mageuzi ya kuboresha sekta hiyo wakati wa kukodisha baadhi ya viwanda hivyo kwa wawekezaji wa kibinafsi. Hii ni kufuatia mgomo wa wafanyakazi 5,000 kutoka viwanda 4 ambavyo ni Chemelil, Nzoia, Muhoroni na Sony kuanza […]

MLIPA USHURU KUGHARAMIA PENISHENI YA WABUNGE

Wakenya wanakabiliwa na uwezekano wa kuongezewa ushuru ili kugharamia malipo ya uzeeni ya wabunge iwapo mswada uliowasilishwa bungeni na mbunge wa Kitui Central Makali Mulu utapitishwa bungeni na kuwa sheria. Mswada huo unalenga masuala kadhaa ikiwemo kuwapa wabunge waliohudumu kwa muhula mmoja muda zaidi wa kulipa malipo yao ya penisheni waliopokea awali, huku wale waliohudumu […]

UHALALI WA JOPO LA KUTIMULIWA KWA GACHAGUA KUBAINIKA

Mahakama ya upeo imeratibiwa hii leo kutoa uamuzi wake kubaini iwapo jopo la mahakama kuu lililoteuliwa kusikiliza kesi ya akubanduliwa afisini kwa aliyekuwa naibu Rais Rigathi Gachagua lilibuniwa kikatiba. Jopo la majaji 4 wa mahamama hiyo ya upeo litatoa uamuzi kuhusu jopo la majaji 3 wa mahakama kuu lililosikiliza na kuamua kwamba Gachagua atimuliwe Oktoba […]

MWONGOZO WA SHA KUSITISHA ‘UTALII WA KIMATIBABU’

Ni huduma za matibabu ambazo hazipatikani nchini pekee ndizo zitagharamiwa na mamlaka ya afya ya jamii SHA nje ya nchi, katika mwongozo mpya ambao umetolewa na mamlaka hiyo katika juhudi za kuziba mianya ya ufisadi na kuhakikisha fedha za umma zinatumika ipasavyo. Katika mwongozo huo, SHA imetangaza kugharamia upasuaji 36 pekee nje ya nchi kama […]

MAN UNITED YAPANGA MKATABA MPYA NA KOBBIE MAINOO

Klabu ya Manchester United imepanga kuzungumza kuhusu mkataba wa muda mrefu na kiungo wake Kobbie Mainoo, baada ya kuonyesha mchango mzuri chini ya kocha Michael Carrick. Mkataba wake wa sasa unamalizika Juni 2027, ukiwemo chaguo la kuongeza msimu mmoja hadi 2028, lakini United wanataka kuanza mazungumzo ya mkataba mpya mapema mwaka huu ili kumhakikishia huduma ya Mainoo kwa muda mrefu. United imedokeza kuwa wanaridhishwa na maendeleo […]