11 WAJERUHIWA RUMOS HILL WEST POKOT
Shughuli za uokoaji zinaendelea katika eneo la Rumos Hills kaunti ya West Pokot kufuatia mkasa wa kuporomoka kwa mgodi na kuwajeruhi watu 11 huku wengine kadhaa wakiwa bado wamekwama kwenye mgodi huo.
Kulingana na shirika la Kenya Red Cross, mansura watatu wako katika hali mahututi, na wanatibiwa katika hgospitali ya rufaa ya Kapenguria walikopelekwa haraka.
Imearifiwa kuwa wanajamii walikuwa wakijihusisha na uchimbaji wa dhahabu kwenye mgodi huo bila idhini ya mamlaka.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 




































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































