WAKENYA WAPEWA NAFASI KUBWA MARATHON YA COPENHAGEN
Wanariadha wa Kenya wanatarajiwa kuwa miongoni mwa washindani wakuu katika toleo la 46 la Copenhagen Marathon litakalofanyika Jumapili nchini Denmark.
Vincent Mutai anaongoza orodha ya wanariadha wa wanaume baada ya kumaliza wa pili mwaka uliopita, ambapo aliweka rekodi yake bora ya saa 2:09:09 katika mbio hizo za mji wa Copenhagen.
Mutai ni sehemu ya kikosi imara cha wanariadha wa kimataifa, huku mwanariadha wa Ubelgiji Lahsene Bouchikhi akiwa Mzungu pekee miongoni mwa washindani wakuu waliowahi kukimbia chini ya saa 2 na dakika 10.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 




































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































