DE ZERBI: HATUJALI KUSHINDA DHIDI YA VILLA ILIYODHOOFIKA
Kocha wa Tottenham Hotspur Roberto De Zerbi amesema hana tatizo lolote na ushindi walioupata dhidi ya Aston Villa licha ya kikosi cha wapinzani hao kuwa na mabadiliko makubwa.
Tottenham walishinda mabao 2–1 katika mechi ya Ligi Kuu ya Uingereza, huku Villa wakifanya mabadiliko ya wachezaji wao muhimu ili kujiandaa na mechi za michuano ya Ulaya.
De Zerbi amesema Tottenham pia wamekumbwa na majeraha mengi msimu huu, hivyo mabadiliko ya Villa hayabadili uhalali wa ushindi wao katika pambano hilo.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 




































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































