LUSAKA AWAHIMIZA VIJANA KUTUMIA MITANDAO KWA MAENDELEO
Vijana katika Kaunti ya Bungoma wamehimizwa kutumia mitandao ya kijamii na majukwaa ya kidijitali kama njia ya kujipatia kipato na kujiendeleza kiuchumi.
Akizungumza katika eneo la Ndengelwa, Gavana Ken Lusaka amewataka vijana kuacha matumizi mabaya ya mitandao na badala yake kuitumia kwa manufaa yao binafsi.
Lusaka ameyasema hayo wakati wa hafla ya uzinduzi wa kituo cha kidijitali katika eneo hilo, akisisitiza umuhimu wa teknolojia katika kuwainua vijana kiuchumi.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 




































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































