#Local News

MASENETA WAKARIRI HAJA YA MAGAVANA KUAGIZWA

Huku mvutano ukiendelea kati ya maseneta na magavana kuhusu uwajibikaji wa matumizi ya fedha za umma, maseneta wamesisitiza umuhimu wa magavana kufika mbele ya bunge hilo kuweka wazi jinsi serikali zao9 zinavyowajibika mahitaji ya umma.

Seneta wa Nairobi Edwin Sifuna, amekariri kuwa kuna maswali mengi kuhusu matumizi ya fedha za umma katika kaunti mbali mbali ikiwemo Nairobi, ambayo gavana Johnson Sakaja ametakiwa kujibu.

Ametetea ripoti ya mkaguzi wa hesabu za serikali kuhusu matumizi hayo.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *