#Local News

KARUA AKOSOA KAULI ZA KAREN NYAMU KWA MWANAFUNZI

Shinikizo linaendelea kuongezeka dhidi ya Seneta mteule Karen Nyamu kufuatia matamshi yake yenye utata dhidi ya mwanafunzi wa Gredi ya Kumi wakati wa kikao cha Seneti.

Kiongozi wa People’s Liberation Party Martha Karua ameyataja matamshi hayo kuwa ya kusikitisha na yasiyokubalika, huku akiungana na viongozi wengine wanaotaka uwajibikaji kuhusu kauli hizo.

Karua amemtetea mwanafunzi huyo akisema Bunge linapaswa kuwa mahali pa kuwahamasisha vijana kuingia katika uongozi na utumishi wa umma badala ya kuwavunja moyo.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *