WATU WANNE WAKAMATWA KUFUATIA WIZI WA PIKIPIKI HUKO TRANSNZOIA
Watu wanne wamekamatwa eneo la Kiminini katika kaunti ya Transnzoia kufuatia wizi wa Piki piki zaidi ya 60.
Maafisa wa polisi katika kaunti ya Transnzoia kwa ushirikiano na wenzao wa kaunti ya Uasin Gishu wamefanikiwa kupata pikipiki hizo ambazo zinaaminika kuibiwa katika wizi wa kimabavu uliosababisha vifo vya watu watano.
Wakaazi wamewapongeza maafisa wa polisi kwa kufanya oparisheni hiyo ambayo wanasema kuwa itaimarisha usalama wao.
Imetayarishwa na Janice Marete
English 




































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































