#Athletics #Sports

OMANYALA AJIANDAA KWA MBIO KALI SHANGHAI

Mwanariadha Ferdinand Omanyala anatarajiwa kushiriki mojawapo ya mbio ngumu zaidi msimu huu atakapowania mbio za mita 100 katika mashindano ya Diamond League Shanghai mwishoni mwa wiki hii.

Nyota huyo wa mbio fupi anaingia katika mashindano hayo akiwa katika kiwango kizuri baada ya kufanya vyema katika mashindano mbalimbali barani Afrika.

Omanyala alianza msimu wa mwaka 2026 kwa mashindano ya ndani kabla ya kushinda mbio zake za kwanza za mita 100 za nje mjini Stellenbosch kwa muda wa sekunde 10.19.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *