#Local News

UDA, DCP KUTOANA KIVUMBI EMURUA DIKIIR 

Wakazi katika eneo bunge la Emurua Dikiir wameendelea kujitokeza kushiriki uchaguzi mdogo wa kumchagua mbunge wao kumrithi marehemu Johanna Ng’eno aliyewaongoza tangu mwaka 2013 eneo bunge hilo lilipobuniwa.

Zoezi la upigaji kura limeanza mapema leo, huku wapiga kura wapatao 44,000 wakitarajiwa kushiriki zoezi hilo linalowaniwa na wagombeaji watano, kivumbi kikali kikiwa baina ya UDA na DCP.

Tume ya IEBC imewahimiza wakazi kudumisha amani wanapojitokeza kupiga kura.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *