MVUA KUBWA YAENDELEA KUSHUHUDIWA TRANS NZOIA
Wakazi wa wadi ya Kiptoro- Chepsiro kaunti ya Trans Nzoia wametakiwa kuchukua tahadhari kutokana na ongezeko la watu kufa maji eneo hilo, watu wawili wakiripotiwa kufariki katika muda wa wiki moja iliyopita.
Naibu chifu wa Kiboswa Gilbert Chepsiror, amesema kisa cha hivi punde kinamhusisha mfanyabiashara mmoja wa eneo hilo, aliyeripotiwa kujirusha katika mto Moiben unaounganisha kaunti hiyo na Uasin Gishu.
Amewahimiza wakazi kusaka ushauri nasaha wanaposongwa na mawazo.
Imetayarishwa na Hilda Ajema
English 






































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































