#Football #Sports

XABI ALONSO AHUSISHWA NA UHAMISHO WA LIGI KUU YA UINGEREZA

Kocha Xabi Alonso ameripotiwa kufungua uwezekano wa kuhamia Ligi Kuu ya Uingereza msimu huu wa kiangazi baada ya mawasiliano ya awali kufanywa kupitia mawakala wake.

Chelsea inadaiwa kuwa na orodha ya makocha wanaowafikiria, huku wakifuatilia upatikanaji wa Alonso pamoja na Andoni Iraola ambaye anataka kuendelea kubaki katika Ligi Kuu ya Uingereza.

Hata hivyo, bado hakuna uamuzi rasmi uliotolewa kuhusu klabu ambayo Alonso anaweza kujiunga nayo katika kipindi kijacho cha uhamisho wa wachezaji na makocha.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *