#Football #Sports

MUYOTI AIPA POLICE IMANI DHIDI YA BANDARI 

Kocha mkuu wa Kenya Police FC, Nicholas Muyoti, amesema ana imani kikosi chake kitaibuka na ushindi watakapovaana na Bandari FC katika nusu fainali ya kombe la Mozzart Bet siku ya Jumamosi.

Muyoti amewataka wachezaji wake kubaki makini, wenye nidhamu na kudhibiti presha ya mchezo huo utakaochezwa katika Nyayo National Stadium.

Mshindi wa mashindano hayo atawakilisha Kenya katika michuano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika msimu ujao.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *