#Football #Sports

ARNE SLOT ATHIBITISHA KUSALIA LIVERPOOL

Kocha wa Liverpool FC, Arne Slot, amethibitisha kuwa ataendelea kuinoa klabu hiyo msimu ujao huku akisema tayari anahusika katika mipango ya usajili wa wachezaji wapya.

Slot amesema ana mkataba na Liverpool na mazungumzo yanayoendelea ndani ya klabu yanaonyesha wazi kuwa atasalia kuwa kocha wa kikosi hicho msimu ujao.

Kauli hiyo imewapa matumaini mashabiki wa Liverpool huku wengi wakiamini mwendelezo wake utaisaidia timu hiyo kujenga kikosi imara kwa msimu mpya wa mashindano.

Arbeloa amtaka Mbappe ajitune zaidi 

Kocha wa Real Madrid, Alvaro Arbeloa, amemtaka mshambuliaji wa Ufaransa Kylian Mbappé kuonyesha kujitolea zaidi kwa timu katika mechi tatu zilizobaki msimu huu.

Mbappe amekuwa akikosolewa na baadhi ya mashabiki wa Madrid baada ya kwenda likizo nchini Italy wakati akiendelea kupona jeraha la paja.

Nyota huyo alikosa mechi ya El Clasico ambapo Madrid walifungwa na FC Barcelona, matokeo yaliyowapa Barcelona ubingwa wa La Liga na kuiacha Real Madrid ikimaliza msimu bila taji lolote.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *