#Local News

GACHAGUA, SIFUNA WADOKEZA KUSHIRIKIANA

Aliyekuwa naibu Rais Rigathi Gachagua na katibu mkuu wa ODM Edwin Sufuna, wamedokeza kuhusu uwezekano wa kushirikiana kwenye uchaguzi mkuu ujao katika azma yao ya kumng’oa mamlakani Rais William Ruto.

Wakizungumza katika kaunti ya Nyeri, wawili hao wamesema muungano wa upinzani utalazimika kuzika tofauti zao iwapo unalenga kutimiza azma hiyo.

Kauli yao inajiri huku utafiti ukionyesha kuwa Rais Ruto ana umaarufu mkubwa miongoni mwa wapiga kura ikilinganishwa na wapinzani wake.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *