#Local News

MWANIAJI WA UDA AIBUKA MSHINDI EMURUA DIKIRR

Mgombeaji wa ubunge katika eneo bunge la Emurua Dikirr kupitia tiketi ya chama tawala cha UDA David Keter, ametangazwa mshindi wa kiti hicho kwenye uchaguzi mdogo ulioandaliwa hapo jana, baada ya kujizolea jumla ya kura 18,266.

Kulingana na tume huru ya uchaguzi na mipaka, IEBC, mgombeaji wa DCP Vincent Rotich alimaliza wa pili akiwa na kura 10,760 baada ya kura za vituo vyote 94 kujumlishwa, IEBC ikisema jumla ya kura zilizohesabiwa ni 29,358.

Wawaniaji wengine 3 walipata chini ya kura 200 kila mmoja.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *