#Local News

KESI DHIDI YA OKOTH OBADO YATUPILIWA MBALI

Aliyekuwa  gavana wa Migori Okoth Obado  watoto wake wanne pamoja na washirika wao wameondolewa mashtaka ya ufisadi wa shilingi milioni 73.5 baada ya mahakama ya kukabiliana na ufisadi ya milimani  kuruhusu ombi la mkurugenzi mkuu wa mashtaka ya  umma la kuondoa kesi hiyo kufuatia makubaliano ya nje ya mahakama.

Katika uamuzi wake hakimu Celisa Okore amesema mahakama imeridhika kwamba ODPP hakutumia vibaya mamlaka yake katika kufanikisha makubaliano hayo na kuyapitisha rasmi kama hukumu ya mahakama.

Imetayarishwa na Hilda Ajema

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *