AFISA ‘ALIYEUAWA’ MAJENGO AFUTWA KAZI, POLISI
Afisa wa polisi anayedaiwa kufyetua risasi na kusababisha kifo cha mvulana mwenye umri wa miaka 17 mtaani Majengo jijini Nairobi amepokonywa bunduki na kusimamishwa kazi huku uchunguzi zaidi ukiendelea.
Haya ni kwa mujibu wa msemaji wa idara ya polisi Michael Muchiri, ambaye amewataka wenyeji kushirikiana na maafisa wa idara DCI na kitengo cha kushughulikia masuala ya ndani kwa ndani wanaofanya uchunguzi.
Aidha, amewataka wenyeji hasa vijana, kudumisha utulivu.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 



































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































