JUBILEE YAMTETEA UHURU KENYATTA KUHUSIANA NA MAANDAMANO
Chama cha Jubilee kimekosoa matamshi ya viongozi wa UDA kwa madai ya kumhusisha rais mstaafu Uhuru Kenyatta na maandamano ya kupinga bei ya mafuta nchini.
Chama hicho kimetaka heshima itolewe kwa rais huyo mstaafu huku kikisisitiza kuwa siasa za lawama hazitasaidia taifa.
Naibu kiongozi wa Jubilee Fred Matiang’i amesema viongozi wanapaswa kuacha kulaumiana na badala yake kujikita katika masuala yanayowahusu wananchi.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 



































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































