#Local News

MBADI AKOSOA WANAOPINGA MSWADA WA FEDHA

Waziri wa Fedha John Mbadi amemkosoa aliyekuwa Waziri wa Usalama wa Ndani Fred Matiang’i pamoja na viongozi wengine wa upinzani wanaotaka Mswada wa Fedha 2026 ukataliwe.

Mbadi amesema viongozi wanaowataka Wakenya kupinga mswada huo wanapaswa kwanza kueleza vipengele wanavyopinga badala ya kutoa matamshi ya kisiasa ya jumla.

Mbadi amesema ni makosa kuwahamasisha wananchi kuandamana dhidi ya mswada bila kutoa mapendekezo mbadala au kueleza kasoro zilizopo ndani yake.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *