#Local News

BUNGE LAKUBALI MAPENDEKEZO YA NDINDI NYORO KUHUSU MAFUTA

Bunge la Taifa limekubali kuyazingatia mapendekezo ya Mbunge wa Kiharu Ndindi Nyoro yanayolenga kupunguza bei ya mafuta nchini.

Kupitia taarifa kutoka Ofisi ya Bajeti ya Bunge, Bunge limethibitisha kupokea barua ya Nyoro ya Mei 15 yenye mapendekezo ya marekebisho ya sheria yanayolenga kupunguza gharama ya dizeli kwa angalau shilingi 54 kwa lita.

Hatua hiyo imejiri wakati serikali ikiendelea na mazungumzo na wadau wa sekta ya uchukuzi kufuatia mgomo wa matatu uliosababishwa na kupanda kwa bei ya mafuta.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *