ARTETA AELEZA FURAHA YA KUTWAA UBINGWA
Kocha wa Arsenal Mikel Arteta amesema kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya England ni moja ya hisia bora kuwahi kupata maishani mwake.
Arteta amesema hakuweza kutazama mechi ya Manchester City lakini alikuwa akisikia kelele kutoka ndani kabla mwanawe kufungua mlango na kumkimbilia huku akilia.
Kocha huyo amesema mwanawe alimwambia kuwa Arsenal wametwaa ubingwa wa EPL kauli iliyogusa wengi baada ya Arsenal kutwaa ubingwa huo baada ya miaka 22.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 



































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































