#Athletics #Sports

ELIUD KIPCHOGE KUSHIRIKI CAPE TOWN MARATHON

Eliud Kipchoge anatarajiwa kushiriki mbio za Cape Town Marathon Jumapili nchini Afrika Kusini  katika harakati za kuongeza historia nyingine katika taaluma yake.

Bingwa huyo mara mbili wa Olimpiki amewasili mjini Cape Town tayari kuipa mbio hiyo hadhi zaidi huku waandalizi wakisaka kuitambua kama mbio za kwanza Afrika kuingia kwenye mashindano ya Abbott World Marathon Majors.

Mashindano hayo pia ni sehemu ya mpango wa Kipchoge wa kukimbia katika mabara yote saba duniani ndani ya miaka miwili ijayo ili kuhamasisha maisha yenye afya kupitia riadha.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *