#Local News

EPRA YAHAKIKISHA HAKUNA UPUNGUFU WA MAFUTA

Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Petroli EPRA imesema Kenya ina akiba ya mafuta ya kutosha kudumu angalau mwezi mmoja licha ya changamoto za usambazaji duniani.

Mkurugenzi wa mafuta na gesi Edward Kinyua amesema nchi ina akiba ya dizeli na petroli ya kutosha pamoja na meli kadhaa zilizoko tayari kushusha shehena katika bandari ya Mombasa.

Ameongeza kuwa pia kuna meli nyingine za mafuta zilizoko pwani ya Mombasa zikisubiri kushusha mzigo ili kuimarisha usambazaji nchini.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *