WAKULIMA WATAKIWA KUTUMIA MBEGU HALALI
Katika juhudi za kuimarisha uzalishaji wa chakula nchini, wakulima wamehimizwa kutumia mbegu kutoka kwa kampuni zilizoidhinishwa na bodi ya udhibiti na ubora wa mbegu KEPHIS.
Akizungumza katika kaunti ya Meru, mkurugenzi wa ubora wa mbegu nchini Simon Maina amesema kuwa serikali ina kesi 15 mahakani kuhusiana na mbegu ghushi, kesi 5 miongoni mwao zikiwa katika kaunti ya Meru.
Naye afisa mkuu wa kilimo kwenye kaunti hiyo James Mutia amewataka wakulima pia kuhakikisha mbegu za miche ikiwemo maembe zimeidhinishwa.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































