MZIGO WA WAFANYIKAZI HEWA WAMLEMEA MLIPA USHURU
Mkenya mlipa ushuru ameendelea kuathirika baada ya tume ya utumishi wa umma (PSC) kugundua wafanyikazi hewa 17,000 wanaogharimu serikali mabilioni ya fedha kila mwaka.
Waziri wa utumishi wa umma, Justin Muturi, amewasilisha mswada wa 2024 wa usimamizi na maendeleo ya utumishi wa umma, unaolenga kuondoa wafanyikazi hewa, kufanya ukaguzi wa mishahara kila robo mwaka, na kuimarisha usimamizi wa pensheni na bima ya matibabu kwa watumishi wa serikali.
Imetayarishwa na Mercy Asami
English 









































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































