#Local News

BUNGE LAPINGA TAARIFA ZA USHURU KWA ARDHI YA UMILIKI WA KUDUMU

Bunge la Kitaifa limekanusha taarifa zinazosambazwa mtandaoni kuwa Mswada wa Fedha 2026 unapendekeza Wakenya kulipa kodi ya kila mwaka kwa ardhi ya umiliki wa kudumu.

Bunge hilo limesema madai hayo ni ya kupotosha na yanalenga kuwachanganya wananchi kuhusu yaliyomo kwenye mswada huo.

Limefafanua kuwa Mswada wa Fedha 2026 hauna kipengele chochote kinachohusu ushuru wa ardhi, umiliki wa kudumu wala kubadilisha ardhi hiyo kuwa ya kukodisha.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *