#Football #Sports

ULINZI STARS WAPANIA KUEPUKA KUSHUKA DARAJA

Kocha wa Ulinzi Stars Mulinge Ndeto amesema timu hiyo itaendelea kupigania kusalia katika Ligi Kuu ya SportPesa hadi mwisho wa msimu.

Kauli hiyo imejiri baada ya Ulinzi Stars kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Mathare United, ushindi uliowapa matumaini mapya ya kuepuka kushuka daraja.

Timu hiyo sasa iko nafasi ya 15 ikiwa na alama 35 huku zikiwa zimesalia mechi mbili muhimu kabla ya msimu kumalizika.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *