KENYA YASHINDWA KUTAMBA CAPE TOWN MARATHON
Mashindano ya Sanlam Cape Town Marathon yalikuwa magumu kwa wanariadha wa Kenya huku nchi ikipata nafasi moja pekee ya jukwaani katika mbio za wanaume na wanawake.
Kalipus Lomwai ndiye aliyekuwa Mkenya pekee kumaliza katika tatu bora baada ya kushika nafasi ya tatu kwa muda wa saa 2:05:06 katika mbio za wanaume.
Mbio hizo zilitawaliwa na wanariadha wa Ethiopia wakiongozwa na Mohamed Esa aliyeshinda kwa rekodi mpya ya mashindano, huku marathon hiyo ikiweka historia kama mbio za kasi zaidi kuwahi kuandaliwa barani Afrika.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































