SERIKALI YA KISUMU YATAKIWA KUFANYA KIPAUMBELE MASWALA YA AFYA
Washikadau katika sekta ya afya ya umma katika kaunti ya Kisumu wametoa wito kwa serikali ya kaunti hiyo kufanya kipaumbele swala la afya ya umma kuhakikisha kwamba mikakati maalumu imewekwa kuimarisha miundomsingi na vile vile kuhakikisha kwamba wahudumu wa afya wa kutosha wanaajiriwa.
Aidha wanamtaka gavana Anyang Nyongo kuhakikisha idara ya afya ya umma inatengewa fedha za kutosha ili kufanikisha utekelezwaji wa shughuli mbali mbali za idara hiyo.
Imetayarishwa na Janice Marete
English 














































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































