GOR MAHIA WATWAA UBINGWA WA LIGI KUU YA FKF
Gor Mahia wametwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya FKF msimu wa 2025/26 baada ya AFC Leopards kufungwa mabao 2-1 na APS Bomet.
K’Ogalo wameweka rekodi mpya kwa kutwaa taji lao la 22 licha ya kutocheza mechi yao dhidi ya Mara Sugar iliyositishwa kutokana na mzozo wa uwanja.
Matokeo hayo yaliiacha AFC Leopards nyuma kwa alama nne huku ikiwa imesalia mechi moja pekee, na hivyo kuthibitisha Gor Mahia kuwa mabingwa rasmi wa ligi.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































