AULIWA BAADA YA KUMUUA MKEWE KWA SABABU YA SHILINGI 30
Maafisa wa upelelezi wanachunguza kisa cha kusikitisha ambapo mzee wa miaka 60 anadaiwa kumdunga kisu na kumuua mkewe katika mzozo wa Sh30 katika kijiji kimoja Kaunti ya Siaya.
Mwanamume huyo aliyetambulika kama Ben Odweso baadaye aliuawa na kundi la watu waliojawa na gathabu baada ya kisa hicho katika kijiji cha Nyalula.
Alidaiwa kumdunga kisu na kumuua mkewe Pamela Anyango mwenye umri wa miaka 55 jana Jumapili kufuatia kutoelewana kuhusu Sh30.
Imetayarishwa na Janice Marete
English 















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































