KWAHERI OTP, INGIA DIJITALI
Shughuli za matibabu chini ya bima ya afya ya serikali SHA zinatarajiwa kurahishwa baada ya serikali kuondoa mfumo wa uthibitisho wa OTP, uliowataka wakenya kusubiri ujumbe kwenye simu zao kabla ya kuhudumiwa.
Akitangaza kusitishwa rasmi kwa mfumo huo, waziri wa afya Aden Duale amesema watumiaji wa bima hiyo watahitajika kujisajili upya kupitia mfumo wa kiidijitali.
Hatua hiyo itarahisisha upatikanaji wa matibabu kupitia SHA mbali na kupunguza ulaghai uliiokuwa ukiendelezwa na baadhi ya hospitali nchini.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 



















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































