RUTO AZUA VICHEKO BUNGENI TANZANIA
Rais William Ruto amewachekesha wabunge wa Tanzania baada ya kueleza kwa utani sababu ya kutumia lugha ya Kiingereza badala ya Kiswahili wakati wa hotuba yake.
Akihutubia bunge hilo, Ruto alitoa maelezo ya kihistoria kwa kuhusu Kiswahili kabla ya kuamua kutumia Kiingereza, akisema hataki kukosea katika matumizi ya lugha hiyo.
Kauli hiyo ilizua vicheko miongoni mwa wabunge, huku ziara yake rasmi nchini humo ikilenga kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia kati ya Nairobi na Dodoma.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 



















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































