KAUNTI KAME ZAPINGA GACHAGUA, KARUA

Viongozi kutoka kaunti kame 15 hapa nchini wamejitokeza kupinga pendekezo la Naibu Rais Rigathi Gachagua na kiongozi wa Narc Kenya Martha Karua linalotaka ugavi wa raslimali za nchi ufainyike kwa misingi ya idadi ya watu katika kila eneo.
Wakiongozwa na spika wa zamani wa seneti Ekwe Ethuro, viongozi hao wamesema mfumo unaopendekezwa ni wa kibaguzi, wakitaka mfumo wa sasa wa raslimali kutolewa kulingana na ukubwa wa eneo kusalia.
Imetayarishwa na: Antony Nyongesa
English 

















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































