RUTO ATAKA MAGEUZI YA HARAKA KATIKA UMOJA WA AFRIKA
Rais William Ruto ametaka kuharakishwa kwa mageuzi ndani ya Umoja wa Afrika ili bara la Afrika liweze kujitegemea zaidi kupitia taasisi imara na ufadhili endelevu.
Rais amesema Afrika lazima ipunguze utegemezi wa nje na kuimarisha uwezo wake wa kushughulikia changamoto zake kupitia utekelezaji wa Ajenda 2063 ya Umoja wa Afrika.
Ruto amezungumza baada ya kuongoza kikao cha nne cha kamati maalum ya wakuu wa nchi kuhusu mageuzi ya Umoja wa Afrika kilichofanyika kwa njia ya mtandao.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 
























































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































