SERIKALI KUANZISHA MFUMO WA MIUNDOMBINU JULAI
Waziri wa Hazina ya Kitaifa John Mbadi amesema Mfuko wa Kitaifa wa Miundombinu utaanza kufanya kazi rasmi mwezi Julai mwaka huu kusaidia kufadhili miradi ya maendeleo nchini.
Mbadi akiwa mbele ya kamati ya bunge kuhusu kawi amesema baadhi ya miradi ya nishati imewekwa chini ya mfumo wa ushirikiano kati ya sekta ya umma na binafsi.
Aidha amesema baadhi ya miradi imehamishiwa chini ya Mfuko wa Kitaifa wa Miundombinu ili kuimarisha utekelezaji wake na kupunguza utegemezi wa mikopo.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 
























































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































