#Local News

MARAGA AKOSOA SERIKALI KWA KUPUUZA MAAGIZO YA MAHAKAMA

Aliyekuwa Jaji Mkuu David Maraga ameikosoa serikali kwa kupuuza maagizo ya mahakama na kuahidi kulinda utawala wa sheria iwapo atachaguliwa kuwa rais.

Akizungumza katika kaunti ya  Turkana Cwakati wa uzinduzi wa kampeni ya Ukombozi, Maraga amesema serikali ya sasa haiheshimu Katiba wala maamuzi ya mahakama.

Amedai kuwa serikali imekuwa ikipuuzilia mbali maagizo ya fidia kwa wananchi waliojeruhiwa kwa kupigwa risasi na maafisa wa usalama wakati wa maandamano.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *