STEPHEN MULE AKOSOA MFUMO WA UAGIZAJI MAFUTA
Mbunge wa Matungulu Stephen Mule amekosoa mfumo wa serikali kwa serikali wa uagizaji wa mafuta akitaka soko huria lirejeshwe.
Mule pia amependekeza kupunguzwa kwa Kodi ya Ongezeko la Thamani kwa mafuta kutoka asilimia 8 hadi 4 ili kupunguza mzigo kwa wananchi.
Akizungumza kwenye mahojiano na kituo kimoja humu nchini, Mule amesema mfumo wa sasa umepunguza ushindani na kuchangia kupanda kwa bei ya mafuta nchini.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 
























































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































