VIONGOZI WA UASIN GISHU WATAKA ULINZI WA RAIS UIMARISHWE
Baadhi ya viongozi kutoka Kaunti ya Uasin Gishu wamekosoa hitilafu ya kiusalama iliyotokea wakati wa ziara ya Rais William Ruto katika Kaunti ya Kilifi.
Viongozi hao wakiongozwa na Gavana wa Kaunti hiyo Jonathan Bii wametaka hatua zaidi kuchukuliwa kuimarisha usalama wa mkuu wa nchi.
Wamesema ni muhimu kuhakikisha matukio kama hayo hayajirudii tena siku zijazo.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 
























































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































