#Football #Sports

ROONEY ONYANGO AITA AFCON 2027 FURSA YA KIPEKEE KWA KENYA

Beki wa kimataifa wa Kenya Rooney Onyango amesema mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika 2027 yatakuwa nafasi ya kipekee kwa soka ya Kenya kuandika historia mpya.

Onyango ambaye kwa sasa anachezea Klabu Sogndal nchini Norway amesema mashindano hayo yatakuwa na uzito mkubwa kihistoria na kihisia kwa wachezaji wa Kenya.

Beki huyo wa kulia mwenye umri wa miaka 24 amesema anaendelea kujituma kurejesha kiwango bora akiwa klabuni huku akijiandaa kusaidia Harambee Stars kuelekea AFCON 2027 ambayo itaandaliwa Afrika Mashariki.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *