KNUT YAAMRISHA WALIMU WA JSS KUREJEA KAZINI
Chama cha kitaifa cha walimu KNUT kimewaagiza walimu wa shule za sekondari ya msingi JSS wanaogoma kurejea kazini.
Katibu mkuu wa KNUT Collins Oyuu anasema chama hicho kiko tayari kufanya mazungumzo na tume ya huduma za walimu TSC kushughulikia malalamiko yao amabyo yamekuwa yakiibuliwa wakisema kwamba wanafunzi wanaangaika na wanasalia nyuma kimasomo.
Oyuu amesema tayari TSC imekubali kuondoa barua walizokuwa wameandikiwa baadhi ya walimu kutaka kueleza ni kwa nini wasichukuliwe hatua kwa kukosa kurejea kazini.
English 





























































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































