RAIS WA CAF AFANYA ZIARA SENEGAL
Rais wa Shirikisho la Soka Barani Afrika (CAF), Patrice Motsepe, amefanya ziara nchini Senegal takriban mwezi mmoja baada ya uamuzi wa kustaajabisha wa kuondoa Senegal kutoka ubingwa wa AFCON na kuutumia Morocco.
Motsepe alitangaza safari hiyo mwishoni mwa Machi akisema atatembelea Senegal na Morocco ili kusisitiza umuhimu wa “kushirikiana kukuza soka barani Afrika,” huku shirikisho lake likikabiliwa na ukosoaji mkubwa.
Rais Bassirou Diomaye Faye atakutana na Motsepe katika Ikulu ya Rais, huku mkutano na waandishi wa habari ukifuata.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 

































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































