UVAMIZI DHIDI YA OSOTSI: DCI YAWAZUILIA WATATU
Washukiwa watatu wanaendelea kuhojiwa na maafisa wa upelelezi baada ya kukamatwa hapo jana kuhusiana na shambulizi dhidi ya seneta wa Vihiga Godfrey Osotsi katika mkahawa mmoja jijini Kisumu Jumatano.
Watatu hao walikamatwa na maafisa wa DCI kutoka Kisumu, uchunguzi wa awali ukionyesha walikuwa miongoni mwa washukiwa wengine wanaoendelea kusakwa.
Kulingana na Osotsi anayeendelea kutibiwa jijini Nairobi, shambulizi hilo lilikuwa jaribio la kumwangamiza.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 

































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































