WAZIRI OGAMBA AZUNGUMZA KATIKA ENEO LA MKASA WA MOTO HUKO GILGIL
Waziri wa elimu Julius Ogamba amesema kati ya wanafunzi 808 ambao walikua katika shule ya wasichana ya Utumishi huko Nakuru wakati wa mkasa wa moto wanafunzi 79 wamejeruhiwa, huku 71 wakihudumiwa na kuruhusiwa kuondoka hospitalini, saba wakiendelea kupokea matibabu.
Akizungumza katika shule ya wasichana ya Utumishi Ogamba ametuma rambi rambi zake kwa familia na marafiki wa wale wanafunzi 16 ambao wameaga dunia kutokana na mkasa huo wa moto akiahidi kuwa wizara yake itaikagua shule hiyo kubaini iwapo ilifuata muongozo wa usalama ambao ni sharti kwa shule za mabweni kufuatwa akisema ripoti hiyo itakapokamilika itawekwa wazi kwa umma.
Imetayarishwa na Hilda Ajema
English 











































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































