#Local News

WANDAYI AHAKIKISHIA NCHI KUHUSU UPATIKANAJI WA MAFUTA

Waziri wa Nishati Opiyo Wandayi amesema Kenya ina akiba ya kutosha ya mafuta licha ya ripoti za uhaba katika baadhi ya maeneo ya ukanda huu kutokana na vita vinavyoendelea Mashariki ya Kati.

Wandayi ambaye alikagua vituo vya mafuta katika kaunti za Nairobi na Machakos amesema serikali imejitolea kuhakikisha usambazaji wa mafuta haukatizwi.

Aidha amewataka wananchi kuwa watulivu akisema bei ya mafuta inaweza kushuka mara hali ya soko la kimataifa itakapotengemaa.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *