#Local News

DCI YAMKAMATA  MUSHUKIWA WA MATAMSHI YA UCHOCHEZI MITANDAONI

 Maafisa wa upelelezi wa kesi za jinai DCI wamemkamata mshukiwa anaehusishwa na matamshi ya uchochezi yaliyokuwa yakisambaa mitandaoni.

Katika taarifa DCI imesema Evans Onyango Kawala maarufu kama Kidero Jasuba amekamatwa katika eneo la Shujaa Mall mtaani Kayole jijini Nairobi.

Kulingana na DCI mshukiwa huyo mwenye umri wa miaka 33 anaendelea kuzuiliwa akisubiri kufikishwa mahakamani hapo kesho.

Imetayarishwa na Hilda Ajema

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *